新浪博客

MAO.DAFU

2023-04-16 11:07阅读:
ULIMWENGU WA KISWAHILI 斯瓦希里语世界 THE SWAHILI WORLD

MASIMULIZI TEULE YA AJABU KUTOKA KWENYE UKUMBI WA SOGA
SELECTED STRANGE TALES FROM CHAT STUDIO
Mwandishi: Pu Songling
Mchapishaji: Shirika la Uchapishaji wa Umma wa Jilin
MAO.DAFU2021年3月由深圳市碧兰星印务有限公司印制
DIBAJI
Pu Songling (1640 1715) alikuwa mwandishi mashuhuri wa fasihi ya kale ya China. Ali
kuwa mwenyeji wa Kijiji chaPujia, Mji wa Zichuan, jimboni Shandong.alizaliwa katika ukoo wa kikabaila uliokuwa ukitopea na kuzorota. Alipokuwa na umri wa miaka 19 alipata shahada ya kwanza na sifa yake ilikuwa kubwa, lakini hakufaulu maishani katika mitihani ya ngazi ya juu iliyofuata, ijapokuwa alijaribu mara nyingi sana. Kwa kuwa hali ya maisha ilikuwa duni, aliwahi kufanya kazi ya utumishi kwa Mkuu wa Wilaya ya Baoying kwa mwaka mmoja na kufanya kazi ya ualimu katika koo za makabaila wakubwa kwa miaka mingi. Maisha yake ya ufukara yalimfanya afahamu ugumu na uchungu wa makabwela; kutokufaulu kwake katika mitihani kulimfanya agundue kasoro za mfumo wa mitihani ya kifalme; kazi za utumishi alizozifanya chini ya mkuu wa wilaya zilimfanya ajionee upotovu wa uwanja wa maofisa. Hivyo alianza kujenga chuki na jamii siku baada ya siku na akawa na mawazo ya kutumaini kuiondolea matatizo jamii hiyo ambayo ilifunikwa kwa giza totoro.
Katika kitabu cha Masimulizi ya Ajabu Kutoka Kwenye Ukumbi wa Soga ingawa mwandishi alieleza habari nyingi kuhusu mashetani na mbweha lakini kwa kweli hadithi hizi zilisheheni simanzi na hasira za Pu Songling kwa jamii ambazo zilijikusanya kifuani mwake. Kitabu hiki kilieleza maisha, mila na mawazo ya watu walioishi katika China ya kimwinyi. Kilifichua uovu na uasherati wa wafalme, maofisa na makabaila wakubwa,hali kadhalika kilieleza umaskini na shida nyingine za watu duni; kilikejeli kasoro za mfumo wa mitihani ya kifalme ya miaka iliyopita; kilisuta ubaya wa mfumo wa ndoa ya kimwinyi na vilevile kilisifu juhudi za wavulana na wasichana katika kujipatia maisha mema.
Mwandishi alichukua hadithi za mapokeo kama msingi wa utungaji wake, na alifanikiwa kutunga hadithi nyingi nzuri. Alikusanya, kuratibu na kutunga hadithi hizi za ajabu siyo kwa sababu aliamini ushirikina, bali kwa kuwa watawala wa Enzi ya Qing waliendesha siasa ya kikatili kuhusu utamaduni. Watu waliothubutu kukosoa siasa za falme aghalabu waliuawa au kutiwa gerezani. Kwa ajili ya kuepukana na majanga, na kuweza kueneza hadithi zake, Pu Songling alitumia njia ya kuzungumzia habari za mashetani na mbweha kumithilisha hali ilivyokuwa katika miaka ya zama zake.
Kitabu hiki ni kimojawapo kati ya vitabu maarufu vya hadithi katika historia ya fasihi ya China. Pu Songling alianza kutunga kitabu hiki tangu alipokuwa na umri wa miaka 20 hivi, na alimaliza kukitunga kimsingi alipokuwa na umri wa miaka 50. Kwa ujumla kina hadithi 490 na zaidi. Miaka 200 imepita tangu kitabu hiki kuandikwa. Kitabu hiki kimewavutia na kuwafurahisha wasomaji. Katika miaka 100 iliyopita, baadhi ya hadithi za kitabuhiki zimetafsiriwa katika lugha za kigeni zaidi ya 20 na kinajulikana sana katika uwanja wa fasihi ya ulimwengu.
Kwa kutumia fursa hii tunashukuru mtaalamu wa Kiswahili PILI MWINYI wa Tanzania aliyepitia muswada mzima wa tafsiri na kutoa maoni yake ya kusahihisha makosa na kuboresha muswada huo. Zaidi ya hayo, tunatoa shukrani kwa mchapishaji CHANG HONG( 宏), makamu wa mhariri mkuu ZHAO YAN(赵 岩), mhariri DING HAO(丁 昊), wachoraji picha GAO ZHENXIANG(高振翔), WANG YAN(汪 艳), PENG TINGYAO(彭婷遥) wa Shirika la Uchapishaji wa Umma wa Jilin (吉林人民出版社)na watu wote wengine waliowahi kutusaidia mnamo muda wo wote wa uchapishaji wa vitabu hivyo.
ULIMWENGU WA KISWAHILI 斯瓦希里语世界 THE SWAHILI WORLD

MASIMULIZI TEULE YA AJABU KUTOKA KWENYE UKUMBI WA SOGA
聊斋志异选
SELECTED STRANGE TALES FROM CHAT STUDIO
Mwandishi: Pu Songling

MAO DAFU
Hapo kale, paliondokea mganga mmoja aliyeitwa Mao Dafu ambaye alibobea katika kutibu majipu huko Safu ya Milima Taihang. Siku moja, aliporejea kwake baada ya kutibu wagonjwa, a1imkuta mbwamwitu mmoja,ambaye alileta kifurushimdomoni, kisha akachuchumaakando ya barabara. Mao alikiokota kifurushi hicho. Baada ya kukifungua aliona mapambo kadhaa yaliyotengenezwa kwadhahabu. Wakati Mao alipokuwa akipigwa na butwaa, alimwona mbwamwitu alikuja mbele yake, akarukaruka na kuivuta kanzu yake mara kadhaa kwa mdomo, halafuakaondoka polepole. Mao hakutiliamaanani, aliendelea na safari yake. Mbwamwitu alirudi akavuta kanzu yake tena.Mao aliona mbwamwitu huyu hana nia mbayaakamfuata. Walitembea kwa muda,wakaingia katika pango moja kubwa. Mao alimwona mbwamwitu mwingine ambaye alikuwa anaugua na amelala ardhini. Mao alipoangalia kwa uangalifu aligundua jipu moja kubwa kwenye utosi wake ambalo limeozana ndani ya jipu hilo mna mafunza wengi. Alifahamu madhumuni yao, akakwanguavitu vichafu vilivomo ndani ya jipu, akalisafisha na kupaka dawa, akaenda zake. Wakati huo, giza ilizidi nambwamwitu alimsindikiza nyuma yake. Walipotembea kiasi cha kilomita mbili hivi waliwakuta mbwamwitu wengine kadhaanao walitaka kumshambulia Mao huku wakilialia.Mao alihofu kupita kiasi. Mbwamwitu yule aliyemsindikiza alipiga mbio chapuchapu na kuingia katika kundi 1a mbwamwitu hao, akaonekana kama anawaambia maneno fulani. Dakika chache tu baadayembwamwitu wote pamoja na yule aliyemsindikiza Mao wakaenda zao. Mao pia aliendelea na safari yake ya kurejea nyumbani.

Chanzo cha jambo hilo hasakilikuwa hivi: Katika wilayahiyo palikuwa na mfanyabiashara mmoja aitwaye Ning Tai ambaye aliuza mapambo ya dhahabu na fedha. Siku moja, aliuawa na jambazi alipokuwa akisafiri njiani. Jambazi huyo hakuachaalama yoyote ya kuweza kujulisha amekwenda wapi. Wakati Mao alipouza mapambo hayo ya dhahabu, sadfaalionwa na mke wa Ning. Basi mke wa Ning alimburura Mao hadi mahakamani. Mao alieleza jinsi alivyoyapata mapambo hayo, lakini hakimu hakusadiki, akaamuru apigwe kwa ubao. Mao hakuwa na njia ya kujitetea, akapigwa bure. Iliyobaki ilikuwa amwombe hakimu kutoa kibali iliaende kuuliza wale mbwamwitu. Hakimu alituma watumishi wawili wa mahakamaniwafuatane naye, walifika mapango ya mbwamwitu moja kwa moja. Walikutambwamwitu hawapo. Walisubirimpaka wakati wa magharibi, mbwamwitu walikuwa bado hawajarejea, basihao watatu waliamua kurejea.

Njiani walipofika nusu ya safari, waliwakuta mbwamwitu wawili ambao kati yao mmoja ana kovu utosini.Mao aliwatambuaakawasalimu kwa heshima na kusema”Majuzi nilipata tuzo yenu lakini leo hiinimekamatwa kwa sababu ya tuzo hiyona kuzuliwa hatia. Leo msipowafahamisha watumishi hawa wawili jambo hilo, nitapigwakwa ubao mpaka kufa baada ya kurejea mahakamani. Mbwamwitu walipomwona Mao amefungwa kwa kamba walivamia watumishi fulifuli. Watumishi hao wawili walichomoapanga wakakabiliana nao. Mbwamwitu waligusa ardhi kwamdomo, wakabweka kwa sauti yajuu. Baada ya kulia mara mbili tatu, kiasi cha mbwamwitu mia wa milimani walijikusanya hukowakawazunga Mao na watumishi, nao waliogopamno. Mbwamwitu walishindana kumfungulia Mao fungato. Baada ya kitambo, watumishi wakafahamu nia yambwamwitu, basi walifungua Mao na mara tu mbwamwitu wote wakaenda zao. Baada yakurejea mahakamani, wale watumishiwawili walimwelezea hakimu waliyoyaona.Hakimu alistaajabu bali hakumwachia huru Mao. Siku chachebaadayehakimu huyo alikwenda nje kusafiri. Mbwamwitu mmoja alisimamabarabarani na huku akiuma kwa meno kiatu kibovu. hakimu huyo alipita na mbwamwitu alipigambio na kumpita hakimu kwa kasi hadi mbele yakeakakiweka kile kiatu kibovu katikati yabarabara. Hakimu alimwamuru mfuasi wake achukue kile kiatu, baada yahapo, mbwamwitu akaenda zake. Aliporejea mahakamani hakimu alimtuma mfuasiwake aende kisirisiri kutafuta mwenye kiatu hicho. Mtu mmoja alisema kuwa katika kijiji kimoja palikuwa na mtu mmoja aitwaye Cong Xin ambaye aliwahi kufukuzwa na mbwamwitu wawili. Mmoja wao aliwahi kukiuma mdomoni kiatu kibovu cha Xin na kuondoka. Watumishi wa mahakama walikwenda kumwita Cong Xinili aje kuthibitisha jambo hilokumbe kiatu kibovu hicho kweli ni chakehivyo walishuku kwamba ni Xin aliyemwua Ning. Hakimu alimhojiXin, akafahamu kweli Xinalikuwa mwuaji. Chanzo cha jambo hilo kilikuwa hivi:Xin alimwua Ning. Baada ya kumwua, alipokonyakiasi kikubwa cha fedha, lakini hakudiriki kupekuapekua zaidi, hivyo hakuona mapambo yale ya dhahabu yaliyofichwa chini ya mavazi, na baadayemapambo hayo ya dhahabu yakachukuliwa na mbwamwitu.

Hapo zamanipalikuwa na mkunga mmoja. Siku moja alipokuwa akirudi nyumbani kwakealimkuta mbwamwitu njiani. Mbwamwitu huyo alimzuia nakuvuta nguo yake kama kwamba anataka kumvutakwenda mahali fulani, mkunga huyo akamfuata,halafu alimwona mbwamwitu jike ambaye alishindwa kujifungua. Mkunga huyo alimsaidia kwa kumkanda. Baada ya kufaulu kumzalisha mbwamwitu jike, mbwamwitu yule dume alimwachamkunga kurejea nyumbani. Siku ya pili, kwa ajili ya kumshukuru, yule mbwamwitu dume alimpelekea nyama ya paa na kuiweka nyumbani mwake.Kutokana na hadithi hizi tunaweza kujua kwamba mambo kama hayo yaliwahi kutokea,bali si mara moja tu.

我的更多文章

下载客户端阅读体验更佳

APP专享